mazingira

mazingira
kwa pamoja tuyatunze mazingira

Wednesday, October 19, 2016

Dr Slaa anaandika!

Mrisho Gumbo,
Naamini hii ID ni ya kwako na hasa kwakuwa kwenye post unaonekana ukizungumza, napata uhakika kuwa ni wewe.

1) Mkuu wa Mkoa, nakuheshimu kwa kuwa cheo chako ni kikubwa sana. Hata hivyo, ulichokifanya leo na " propaganda unazopiga zimenifanya nikudharau na kukupuuza. Ningeliweza kuishia katika kukudharau na kukupuuza, lakini

2) Aibu uliyoiletea Taifa letu leo, inanifanya " nipige kelele" kuwa " siasa za maji taka siyo wakati wake huu.
a) Mhe.Mrisho Gumbo, wewe kama Mkuu wa Mkoa unayo au mamlaka au vyombo vya dola kukusaidia kufanya utafiti wa maana kuliko aibu kubwa uliyoiletea Taifa letu mbele ya Wahisani/ Wafadhili wetu kupitia Maternity Africa. Hukufanya hivyo, umeamini propaganda kuliko busara na hekima. Kwa hilo siwezi kukusamehe wala kukuheshimu pamoja na cheo au vyeo vyote ulivyonavyo.

b) Mrisho Gumbo, ungelikuwa wa busara iwapo ungelimwomba kiongozi au mwakilishi wa ADF ( ulikuwa na uwezo wa kujua ADF ni nani na historiaya yake ni ipi- kwa kupenda propaganda hukufanya hivyo) au Mwakilishi wa Maternity Africa hasa Happy ( ambaye alisaini pia barua ya kukualika kuwa mgeni rasmi, au hata Mhe. Mbunge Lema ambaye kimsingi ndiye chimbuko la upatikanaji wa Ardhi hiyo kutoka kwa Marehemu Advocate Mawala ( Mwenyezi Mungu amlaze mahala pema peponi), na pia chimbuko la Upatikanaji mradi kutoka kwa wafadhili wetu. Kutokupenda kushauriwa na hao wenye kujua mradi imekufanya "kuonekana ****" na " mwongo" kwa kuwa historia haifutwi kwa " propaganda za jukwaani". Lakini kwa bahati mbaya athari ya propaganda imeenda mpaka kuichafua Taifa letu kwa wahisani. Ujenzi ndiyo kwanza unaanza. Umeombwa kufanya "Ground Breaking ceremony", unadhani wawakilishi wa wahisani na hasa kule kwenye chimbuko la fedha wanapata picha gani ya Taifa letu.

c) Mrisho Gumbo, busara na hekima ya kawaida ingelikuwezesha kuelewa barua ya mwaliko ambayo imesisitiza mara mbili hivi, kuwa wahusika ni taasisi isiyojihusisha na siasa. Wakasema mradi kwa muda sasa umekumbwa na matatizo yenye sura ya kisiasa. Ulipaswa kutafakari, kutafiti na kutafiti njia makini zaidi ya kuona wakina mama wajawazito, wenye fistula na watoto wachanga hawakosei au hata hawacheleweshewi kupata huduma hiyo kwa sababu za kipuuzi tu. Eti unasoma historia! Unsijua historia au unaota ndoto! Nimepiga kelele kwa kuwa ninaijua vizuri hiyo historia A to Z. Sikuambii ungeliniuliza, lakini wapo kwenye kikao hicho ambao wasingelihitaji kuisoma bali kuitoa kichwani historia hiyo, tangu kupatikana kwa Ardhi, mchakato wa kuchora ramani, kuisajili na kupata vibali vyote vya Kituo hicho cha Afya( japo kwa kweli ni hospitali ( inaitwa kituo cha Afya tu kwa. Sababu za kisheria).

3) Mrisho Gumbo, kwa hili Watanzania wa Arusha na wote wenye kujua ukweli hatutakusamehe kwa aibu uliyotupatia, na kujenga misingi ya kutufungia miradi mingine kwa wahisani wetu. Kama una chembe dogo la busara:

a) Utakaa chini na kutafakari umekosea wapi. Ikiwa lazima

b) uwe na unyenyekevu uwaite wahusika wote ofisini kwako waombe wakupe " historia kamili" na wakupe mchakato mzima mpaka kufikia siku hii muhimu ya " Ground Breaking ceremony( uzinduzi wa Kazi ya ujenzi).

c) Ukipata Taarifa kamili, uwe na unyenyekevu, acha kiburi. Kiburi hakikusaidii wala haitasaidia jamii unayopaswa kuwatumikia ( unless una malengo tofauti). Kwa unyenyekevu mkubwa Waombe msamaha Wahisani wetu kwa kuwaingiza katika " siasa ya Arusha" ambayo hawahusiki nayo; awaombe msamaha wakina mama, watoto na jamii ya Wananchi wa Arusha wapenda maendeleo kwa kuwachafua na kuwaletea vurugu kiasi cha kuifanya Arusha ionekane kila leo ni mahali pa vurugu, kumbu vurugu husababishwa na viongozi wasiotumia busara na hekima. Uongozi ni busara na hekima siyo mabavu wala nguvu ya mamlaka.

Nimeyasema haya kuuchungu mkubwa. Mimi siko kwenye siasa, na wala sina interest na siasa. Siangalii uso w a mtu. Kama ambavyo niliaga kuwa " Nastaafu Party Politics, lakini nitapiga kelele pale maslahi ya Taifa langu yanavyokanyagwa" nitakuwa mwendawazimu kunyamaza wakati mradi wa Tshs Takriban 9 Billioni unahatarishwa na upuuzi na uzembe wa kiongozi mnoja mwenye kuendekeza propaganda zisizo na msingi.

Nawaomba sana Radhi wahisani wetu. Mtuvumilie siyo kwa ajili yetu bali kwa ajili ya kina mama na watoto walengwa wa huduma itakayotolewa na " Kituo cha Mama na Mtoto" ( propaganda ya Hospitali ya mke wa Lema zipuuzeni). Happy, umevumilia mengi katika miradi mingi uliyofadhili na kuisimamia. Usirudi nyuma. Timiza ndoto yako iliyoanza katika umri mdogo sana. Matunda yanaonekana pamoja na vikwazo vya mara kwa mara vya wapinga maendeleo. Viongozi, " Tenganisheni siasa na Maendeleo" Watumikieni Watanzania bila kuangalia nyuso zao, mrengo wao. Siasa ni sayansi na siasa sayansi ni utumishi.

By Dr Slaa
Source:Chingaone/Jamii Forums

Babutale amezijibu shutuma za baadhi ya mashabiki nchini kuwa wasanii wa WCB wamekuwa wakinunua tuzo.

Akiongea na Prince Ramalove wa Kings FM, Tale alikuwa na maneno mafupi tu kuwajibu. “Kama ni rahisi na wao wakanunue,” alisema meneja huyo.

Jumamosi iliyopita Diamond na Harmonize walishinda tuzo za Afrimma zilizofanyika jijini Dallas, Marekani.

Alidai kuwa tuzo hizo ni za Tanzania nzima na imeonesha jinsi gani mashabiki wako nao pamoja. Amesisitiza kwa kuwaomba waendelee kuwapigia kura wasanii wote waliotajwa kwenye tuzo za MTV MAMA wakiwemo wasanii wake wa WCB, Diamond na Raymond.

Wengine ni Alikiba, Navy Kenzo, Yamoto Band na Vanessa Mdee.

Mahakama ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam leo imemfutia shtaka la  unyang’anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete maarufu kwa jina la Scorpion baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani hapo kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani anatuhumiwa kumchoma visu na kisha kumtoboa macho, Said Ally mkazi wa Mabibo Hostel hivi karibuni.

Muuza sura kwenye video za Kibongo, Lulu Abass ‘Lulu Diva’ (pichani juu) na mwenzake Amber Lulu (pichani chini) hawana bifu lolote isipokuwa kuna watu wana mpango wa kuwagom-banisha.

Akichonga na Risasi Vibes, Lulu Diva alifunguka kuwa awali aliposikia kuwa Amber alimpaka matope kwenye ‘interview’ aliyofanya na redio fulani Bongo, alipaniki na kumtafuta ili amueleze kulikoni, lakini Amber alimwambia hakuna kitu kama hicho na kumtaka kuchunguza mwenyewe.

“Nilichunguza na kukuta kumbe si kweli, niligundua ni watu wasiopenda ushoga wetu ndiyo walikuwa wanajaribu kutukosanisha na si vinginevyo,” alisema Lulu Diva.

Mahakama Yamfutia Shtaka la Unyang’anyi wa Kutumia Silaha Scorpion


Mahakama ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam leo imemfutia shtaka la  unyang’anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete maarufu kwa jina la Scorpion baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani hapo kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani anatuhumiwa kumchoma visu na kisha kumtoboa macho, Said Ally mkazi wa Mabibo Hostel hivi karibuni.

Tuesday, August 23, 2016

Lowassa Apigilia Msumari Oparesheni UKUTA, Asema Haiwezekani Mtu Mmoja Azuie Kila Kitu

Leo nimezunguka katika majimbo ya Mbeya Vijijini ,Vwawa na Tunduma nikiwaeleza kuhusu Operation UKUTA,

UKUTA si fujo , UKUTA si machafuko na hatuna haja ya kufanya fujo , tunapiga kelele dhidi ya uvunjwaji wa haki ya kidemokrasia na katiba ya nchi unaofanywa na utawala huu wa awamu ya tano .

CHADEMA ni nani wakapambane na polisi ,polisi ambao ni watoto wetu ,ndugu zetu na hata wake na waume zetu ila tuwahakikishie hatutorudi nyuma pale katiba na haki ya kidemokrasia ikichezewa au kuwa chini ya mtu fulani .

Najua polisi watapiga watu ,wataumiza watu na hata kuua ila niwahakikishie wao na walio na mamlaka wataishia katika mahakama ya Kimataifa .

Siasa ni mazungumzo ,lazima tuzungumze milango yetu iko wazi kufanya mazungumzo ila kwa kuwa hawahitaji na sisi hatutorudi nyuma September Mosi ,tumejiandaa vya kutosha na sasa tuko ngazi ya kaya na wajumbe wetu wanakamilisha kazi katika kaya ili tarehe mosi sauti ya kutosha ipazwe kwa maandamano na mikutano kama tulivyokubaliana katika kata zetu na majimbo nchi nzima .

Haiwezekani hata kidogo mtu mmoja azuie kila kitu ,nchi hii ni mali yetu sote na inaongozwa na Katiba na sheria.

Kamati kuu ilipoamua katika suala la UKUTA haikukurupuka , kamati kuu yetu inaundwa na mchanganyiko wa wasomi wa kada mbalimbali ,wazee wenye busara na vijana machachari kamwe hawawezi kukukurupuka na UKUTA ni haki ya watanzania wote.

Pili naomba niwape siri ya ushindi 2020 ndugu zangu na wanachama wenzangu , tutashinda uchaguzi Mkuu 2020 kama tutafanya yafuatayo na kuyasimamia
Kwanza; Umoja ndani ya Chama na wanachama ,tuheshimiane ,tusameheane na tuimarishe chama chetu
"chama ndani ya Chama , chama nje ya chama na chama ndani ya Umma "- LOWASSA

Makundi yayumbisha CCM


KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jijini Arusha, Medest Meikoki amesema kuyumba kwa chama hicho katika Jiji la Arusha na kusababisha upinzani kuongoza kutokana na makundi yaliyopo ndani ya chama hicho.

Akizungumza mjini hapa jana, Meikoki alisema aliamua kustaafu siasa baada ya kusulubiwa na makundi hayo ambayo kwa kiasi kikubwa yalikuwa na nguvu katika miaka ya 2000.

Alisema katika jiji hili kulikuwa na makundi mawili ya G7 na G13 ambayo yalikuwa na nguvu katika miaka hiyo.

Kada huyo, alisema bado baadhi ya wana CCM waliojeruhiwa na makundi hayo wana hasira dhidi ya chama chao na kuamua kukaa pembeni na kuacha wenye pesa wafanye watakavyo, lakini waliapa chama hakitachukua jimbo hilo kamwe.

Alisema hatua za ziada zinatakiwa kuchukuliwa na viongozi wa juu wa CCM wa kuwarudisha kundini waliojeruhiwa na makundi hayo bila ya sababu za msingi vinginevyo, upinzani utaendelea kuongoza.

Kada huyo aliendelea kusema kuwa makundi ya kisiasa ya G7 na G13 ndiyo yamekivuruga chama na kuifikisha siasa ya Arusha kuwa taabani kwani waliokuwa wakichaguliwa walikuwa ni viongozi wasiokuwa na sifa za kuongoza chama hicho.

Alisema, kundi la G7 lilikuwa kundi lenye uwezo mkubwa wa kifedha ambapo wafanyabiashara wakubwa wa Arusha, walikuwa katika kundi hilo na walikuwa wakiamua wanavyotaka na ukipingana nao unang’olewa.

Kada huyo alisema, kundi la G13 lilikuwa kundi la wanasiasa wenye kujua siasa za Arusha na nchi kwa ujumla na walikuwa wapambanaji lakini walikuwa ni watu wa kawaida tu wasiokuwa na fedha, lakini wenye mikakati ya kutaka chama kishike hatamu.

Alisema yeye aliwahi kushughulikiwa mwaka 2000 ndani ya chama na kundi la G7 kwani katika kura za maoni za ndani ya chama, alishinda lakini kundi hilo halikuridhika na likaamua kumtoa mwanaCCM na kumsimamisha upande wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) ili kupambana naye kwenye udiwani wa kata ya Darajambili.

Kada huyo alisema kundi hilo lilifanikiwa, kwani TLP ilishinda katika kiti cha udiwani katika kata hiyo na yeye kuanguka vibaya ingawa awali alishinda kwa kishindo katika kura za maoni ndani ya chama

Alisema baada ya kushughulikiwa mwaka 2000 aliamua kujikita katika kushauri badala ya kugombea na alipoamua kuingia tena kwenye siasa mwaka 2005, alishughulikiwa tena na akaamua kustaafu na kubakia kuwa mshauri hadi sasa.