mazingira

mazingira
kwa pamoja tuyatunze mazingira

Friday, October 28, 2016

Sumaye: Sirudi CCM hata waninyang’anye Mashamba Yangu Yote

Siku moja baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kutangaza nia ya Serikali kumnyang’anya shamba Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, mwanasiasa huyo mkongwe amedai hilo halimtikisi.

Sumaye ambaye tayari ameshakabidhiwa notisi ya siku 90 kutokana na kutoliendeleza, amesema kuwa tayari suala hilo ameshaliwasilisha mahakamani na kwamba mwanasheria wake ndiye anayefahamu tarehe iliyopangiwa kesi hiyo.

“Nilienda mahakamani na ikaamuriwa kusiwe na shughuli yoyote, nasubiri tarehe ya kesi ambayo mwanasheria wangu ndiyo anaijua,” Sumaye anakaririwana MwanahalisiOnline.

Mwanasiasa huyo aliyehamia Chadema miezi michache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka jana, amesema kuwa kama CCM wanataka kumdhoofisha kwa kumnyang’anya mashamba ili arejee haitawezekana.

“Kama walidhani kwa kunifanyia hivi nitarudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) wasahau, hata kama nilikuwa na nia hiyo sirudi,” amesema Sumaye.

Serikali imetangaza kuanza mchakato wa kumnyang’anya Sumaye shamba lake lililoko Mwabwepande jijini Dar es Salaam kwa madai kuwa ameshindwa kuliendeleza kwa muda mrefu, kinyume na matakwa ya sheria.

NATO; hatutaki mzozo na Urusi


Mkuu wa Nato Jens Stoltenberg.Image copyrightAFP
Image captionMkuu wa Nato Jens Stoltenberg.
Nato haitafuti mzozo na Urusi wala haihitaji vita vingine baridi kwa mujibu wa katibu mkuu wa jumuiya hiyo, Jens Stoltenberg.
Stoltenberg anasema kuwa mipango ya kupeleka wanajeshi 4000 zaidi mashariki mwa Ulaya ina lengo la kuzuia badala ya kuzua mzozo.
Licha ya kuwepo misukosuko, muungano wa Nato hautambui Urusi kuwa tisho.
Uhusiano kati ya nchi za magharibi na Urusi umekuwa mbaya zaidi tangu vimalizike vita baridi.
Marekani na Muungano wa Ulaya walikuwa wameiwekea Urusi vikwazo kufuatia hatua yake ya kuimega rasi ya Crimea mwaka 2014.
Rais wa Urusi Vladimir Putin
Image captionRais wa Urusi Vladimir Putin
Vita ncchini syria navyo vimeluwa chanzo cha misukosuko, huku mataifa mnakubw ayaliilaju Urusi wa kuendsha uhalifu wa kivita inapioshgambualia ameneoa yanayodhibitiwa na uopiannai ikiisadia serijali.
Vikosi vya kimataifa vinavyo jumuisha wanajeshi 1000 katika kila kikosi vitapelekwa nchini Poland, Latvia na Lithuania mapema mwaka ujao.
Vikosi hivyo vitaongozwa na Marekani, Uingereza, Canada na Ujerumani.
Nato inasema inaamini kuwa Urusi ina takriban wanajeshi 330,000 walioa karibu na mashariki ya mpaka wake.
Mapema wiki hii mipango ya meli za kivita za Urusi kutia nanga katika bandari ya Uhispania ilivutwa baada ya washirika wa Nato kuelezea wasi wasi kuwa zitatumiwa kushambulia raia nchini Syria.

Afisa aliyemtisha mwandishi wa habari aomba msamaha Kenya


Dola milioni 50 zimetoweka kutoka wizara ya afyaImage copyrightAFP
Image captionDola milioni 50 zimetoweka kutoka wizara ya afya
Afisa wa serikali ambaye ni katibu katika wizara ya afya Nicholas Muraguri, ameomba msamaha kwa kumtisha mwandishi wa habari ambaye alikuwa akichunguza ufisadi kwenye serikali.
Siku ya Jumatano gazeti la Business Daily lilifichua kuwa dola milioni 50 zimetoweka kutoka kwa bajeti ya wizara ya afya.
Kwa mfano dola milioni 7.9 ambazo zilistahili kununua zahanati za afya za kuhama hama hazijulikani ziliko.
Akijibu, bwana Muraguri alimwambia mwandishi huyo wa habari kuwa serikali ina majasusi katika kampuni ya Nation, ambayo huchapisha gazeti la Business Daily.
"Hauielewi serikali, tunaweza kukipata unachokiandika hata kabla hujakichapisha, ikiwemo kupata picha za taarifa. Kama kuna haja ya kudukua mtadao wa Nation tunaweza kufanya hivyo. Tunaweza hata kukuambia ni pesa ngapi ziko kwa akaunti yako."
Kisha afisa huyo akakumbwa na lawama kwa matamshi yake hatua iliyosababisha yeye aombe msamaha.
"Matamshi yangu ni ya kusikitisha na kujutia na hayaonyeshi msimamo wangu kama mfanyikazi wa serikali."

Ndege ya mgombea mwenza wa Trump yapata ajali

Mike PenceImage copyrightAP
Image captionMike Pence (kati) atembea kutoka ndege iliyokuwa imembeba uwanja wa LaGuardia jijini New York
Mgombea mwenza wa chama cha Republican katika kinyang'anyiro cha urais nchini Marekani Mike Pence amenusurika baada ya ndege iliyombeba kuteleza uwanja wa ndege.
Ndege hiyo iliteleza na kuvuka barabara inayotumiwa na ndege kupaa na kutua katika uwanja wa LaGuardia jijini New York.
Gavana huyo wa Indiana amewaambia wanahabari kwamba yuko salama baada ya kisa hicho.
Hakuna aliyejeruhiwa.
Bw Pence na abiria wengine takriban 30 waliokolewa kupitia mlango wa dharura wa ndege upande wa nyuma.
Alikuwa anatoka mkutano wa kampeni Fort Dodge, Iowa.
Uwanja wa ndege wa LaGuardia kwa muda usiojulikana, maafisa wamesema.
Rubani anadaiwa kukanyaga breki na abiria wanasema walinusa harufu ya raba ikiungua.
Ndege ya Pence
Image captionNdege hiyo iliyombeba Pence hatimaye ilisimama kwenye maeneo yenye nyasi
Kanda za video za runinga zimemuonesha Bw Pence baadaye akiwa amesimama kwenye mvua karbu na magari ya huduma za dharura, akizungumza na baadhi ya maafisa.
Baadaye aliandika kwenye Twitter: "Nashukuru sana kwamba kila mtu aliyekuwa kwenye ndege yetu yuko salama. Nashukuru maafisa wa dharura na wote waliotuombea. Tutarejea kwenye kampeni kesho!"
Clinton tweetImage copyrightTWITTER
Amesema matope yaliruka na kujaa kwenye kioo cha sehemu ya mbele ya ndege.
Mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump alimpigia simu Bw Pence kumjulia hali baada ya kisa hicho, maafisa wa kampeni wamesema.
Mike PenceImage copyrightAP
Image captionMr Pence (kati) azungumza na wazima moto LaGuardia
Msemaji wa Trumo Stephanie Grisham alisema mgombea huyo alikuwa kwenye msafara wa kampeni akielekea Geneva, Ohio.
Bw Trump alizungumzia ajali hiyo kwenye mkutano wake wa kampeni baadaye akisema: "Mnajua, kulitokea ajali kubwa ya ndege.
"Ndege imeteleza kutoka barabara uwanja wa ndege na ilikaribia sana kuwa mbaya, kuwa mbaya sana, nimezungumza na Mike sasa hivi na yuko salama. Alitoka. Kila mtu yuko salama."
@mike_penceImage copyrightTWITTER
Image captionMike Pence alikuwa amepakia picha hii kwenye Twitter awali
Bw Pence aliahirisha hafla ya kuchangisha pesa ambayo ilifaa kuandaliwa katika jumba la Trump Tower eneo la Manhattan, na akaelekea moja kwa moja hadi hotelini.
Haijakuwa wiki njema kwa gavana huyo wa Indiana.
Jumatano, alitangaza kwenye Twitter kwamba mbwa wake kwa jina Maverick, alikuwa amefariki akiwa na miaka 13.

Jeshi la Nigeria lawaachilia watoto 876


Wanajeshi huwazuilia raia ambao wamekuwa wakiishi maeneo ya wanamgamboImage copyrightGETTY IMAGES
Image captionWanajeshi huwazuilia raia ambao wamekuwa wakiishi maeneo ya wanamgambo
Umoja wa Mataifa umefanikisha kuachiliwa kwa watoto 876 wanaozuiliwa na wanajeshi wa Nigeria na vikosi vya usalama baada ya kuteka ardhi iliyokuwa ikikaliwa na Boko Haram.
Watoto hao wamekuwa wakizuiliwa katika kambi za kijeshi kwenye mji wa Maiduguri ulio Kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Wanajeshi huwazuilia raia ambao wamekuwa wakiishi maeneo ambayo yamekuwa yakikaliwa na wanamgambo wa kiislamu, kwa kuwashukuwa kwa wana uhusiano na shughuli za wanamgambo hao.
Hata hivyo makundi ya kibinadamu yanalalamika kuwa hakuna sheria ya kuwafungulia mashtaka watu hao.
Baadhi yao hupelekwa kwa vituo vya kurekebisha tabia ambavyo makundi ya kibinadamu yanasema kuwa vinafanana na magereza.

Ubalozi wa Marekani Nairobi wafungwa kwa muda

Mwanamume huyo aliuawa kwa kupigwa risasi kichwaniImage copyrightAFP
Image captionMwanamume huyo aliuawa kwa kupigwa risasi kichwani
Ubalozi wa Marekani nchini Kenya umefungwa kwa muda leo Ijumaa kufuatia kisa ambapo mwanamume aliyekuwa na kisu alijaribu kumshambulia afisa wa usalama karibu na ubalozi huo Alhamisi.
Mwanamume huyo aliuawa kwa kupigwa risasi.
Hakuna afisa yeyote wa ubalozi huo aliyeathiriwa na kisa hicho.
"Ubalozi utafungwa Oktoba 28. Huduma zote za kibalozi zimesitishwa, lakini huduma za kibalozi za dharura kwa raia wa Marekani zitaendelea kutolewa," taarifa kwenye tovuti ya ubalozi huo imesema.
Maafisa wa ubalozi huo wametoa wito kwa raia na wafanyakazi wake kuwa makini kuhusu usalama wao.
Polisi nchini Kenya wanachunguza kubaini iwapo mwanamume huyo aliyepigwa risasi alikuwa na washirika, afisa mmoja mkuu wa polisi Vitalis Otieno aliambia shirika la habari la AFP.
Bw Otieno alisema mwanamume huyo alimdunga kisu afisa mmoja wa polisi lakini akapigwa risasi na kichwani na kuuawa na afisa aliyekuwa karibu.
Maafisa watano wa idara ya uchunguzi wa jinai ya Marekani (FBI) walifika eneo la tukio muda mfupi baadaye pamoja na polisi wa Kenya kufanya uchunguzi.
Msemaji wa polisi Kenya George Kinoti alisema mwanamume huyo wa miaka 24 alikuwa "mhalifu wa kuendesha shughuli zake kivyake", kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters.
Hata hivyo, alisema uchunguzi unaendelea

Duterte: Nimeisikia sauti ya Mungu


Rodrigo DuterteImage copyrightAP
Image captionRais wa Ufilipino Rodrigo Duterte
Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte, ameahidi kuacha kutumia lugha ya matusi baada ya kile anachosema kuwa ni kupata ujumbe wa moja kwa moja kutoka kwa Mungu.
Rais huyo, alliyemwita Rais Barack Obama "mwana wa kahaba" na akasema kiongozi huyo anaweza "kwenda jehanamu", amesema amefikia uamuzi huo baada ya kupata ufunuo alipokuwa safarini kutoka Japan.
Amewatusi pia watu wengine mashuhuri. Alimwita kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis "mwana wa kahaba" (Ufilipino ni taifa lenye Wakatoliki wengi).
Amewahi kumtusi pia waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry kwa kumuita "mwendawazimu" na majuzi alimweleza balozi wa Marekani nchini Ufilipino kama "mpenzi wa jinsia moja ambaye ni mwana wa kahaba".
Bw Duterte amesema kuwa alipokuwa kwenye ndege, na watu wengine wote walikuwa wamelala, alisikia sauti ikimuonya: usipokoma, nitaiangusha ndege hii.
Amesema sauti hiyo ilijitambulisha kuwa ilitoka kwa Mungu.
Amewaahidi watu waliokusanyika mji wake wa nyumbani wa Davao kwamba ahadi kwa Mungu ni sawa na ahadi kwa Wafilipino.
Rais Duterte ni kiongozi ambaye msimamo wake na matamshi yake huzua utata mara kwa mara.
Amesomea taaluma ya sheria na alipanda cheo hadi kuwa mwendesha mashtaka kabla ya kuteuliwa kuwa naibu meya wa Davao wakati wa mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Ferdinand Marcos mwaka 1986.
Alikuwa meya mwaka 1988 na kushikilia wadhfa huo kwa kipindi cha miaka 10, kabla ya kushinda kiti cha ubunge katika Bunge la Congress halafu akarejea kwenye kiti cha umeya mwaka 2001.
Alijijengea umaarufu kwa kupiga vita baadhi ya matatizo makubwa yanayowakabili Wafilipino - uhalifu, makundi ya uasi, na ufisadi. Yote haya yalipungua kwa kiwango kikubwa wakati alipokuwa kiongozi wa Davao, na kufanya mji huo kuwa mmoja wa miji salama zaidi nchini Ufilipino.
Rodrigo Duterte akiwa DavaoImage copyrightREUTERS
Image captionBw Duterte amesema anataka kuokoa Ufilipino kwa ajili ya vizazi vijavyo
Duterte ambaye utawala wake ni wa kipekee kwa kuwa kiongozi mwenye sera za Kijamaa na mwanamageuzi kwa pamoja, sera zake za uchumi zilikuwa si za kuaminika wakati wa kapeni.
Majuzi, alilinganisha vita vyake dhidi ya walanguzi wa mihadarati na mauaji ya Wayahudi wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia.
Alisema anaweza kuua walanguzi wengi wa dawa hizo za kulevya sawa na alivyofanya Hitler akiua Wayahudi.
"Hitler aliua Wayahudi milioni tatu ... kuna waraibu milioni tatu wa dawa za kulevya. Ninaweza kufurahia sana kuwaua," amesema.
Wayahudi zaidi ya milioni sita waliuawa na Wanazi chini ya Hitler.